Ramaphosa ahimiza "mshikamano wa mataifa" mkutano wa G20

 


Mkutano wa kilele wa kundi la mataifa tajiri na yale yanayoinukia kiuchumi duniani la G20 umefunguliwa rasmi siku ya Jumamosi mjini Johannesburg, Afrika Kusini.

Mkutano huo wa siku mbili unafanyika chini ya kiwingu cha kutohudhuriwa na viongozi wengi wa dunia na mjadala mkali kuhusu mpango wa Marekani wa kumaliza vita vya Ukraine.

Rais Donald Trump wa Marekani pamoja na viongozi wa Urusi na China - Vladimir Putin na Xi Jinping - ni miongoni mwa viongozi waliositisha mipango ya kushiriki mkutano huo wa G20 unaofanyika kwa mara ya kwanza barani Afrika.

Viongozi wa Mexico na Argetina pia hawahudhuria mkutano huo huku Rais Bola Tinibu wa Nigeria amelazimika kuifuta safari yake ya kwenda kushiriki mkutano huo ili kushughulia mkasa wa kutekwa wanafunzi zaidi ya 300 na makundi ya watu wenye silaha kaskazinji mwa nchi yake.

Utawala wa Trump umesusia mkutano huo kwa sababu unaituhumu serikali ya Afrika Kusini kwa kufanya ukandamizaji dhidi ya jamii ya wazungu wachache wa nchi hiyo.

Afrika Kusini imekanusha madai hayo ikisema haya msingi wala ushahidi.

Mwenyeji wa mkutano huo wa kilele wa G20, Rasi Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini anatoa kipaumbele kwa mada za mshikamano, usawa na maendeleo endelevu.

Amesema atatumia mkutano huo kupigia debe kupunguzwa mzigo wa madeni kwa mataifa yanayoendelea, usawa katika kuhamia kwenye nishati safi zisizoharibu mazingira, matumizi ya haki ya madini adimu, upatikanaji chakula na mgawanyo wa haki wa majukumu ya kulinda mazingira duniani.


Post a Comment

Previous Post Next Post