Amesema kuondoka kwake ni kugumu lakini hiyo ni mipango ya Mwenyezi Mungu na kutaka Watanzania kulipokea jambo hilo.
“Sisi wanadamu tunapanga lakini Mungu naye anapanga yake, kazi ya Mungu haina makosa, tumshukuru kwa uhai na zawadi ya maisha yake, tutaendelea kumuombea na kuiweka familia yake kwenye maombi.
Rais amesema Tanzania itatafuta mgombea mwingine mwenye sifa zinazoweza kushindana na ulimwengu na kuingia tena kwenye ushindani kwa nguvu ile ile ili kuweka heshima ya nchi.
Alisema ni wajibu wa nchi kuhakikisha Watanzania wabobezi wanawekewa nguvu ili waweze kuwakilisha katika fani za kimataifa kama walivyofanya kwa Dk Ndugulile.
“Mheshimiwa Dk. Ndugulile aligombea, Serikali ikamuunga mkono na akapata,hata hivyo Mwenyezi Mungu hakutaka iwe hivyo na leo tunamuaga mwenzetu na hatujui sisi safari yetu ni lini maana tunakuja na kuondoka”, alisema.



